Search
Sign In
2Your Cart
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Maria Sebastian wa Kawe Mwanamke Mwenye Elimu ya Juu Anayejitolea CCM

  • 26
Scroll Down To Discover

Maria Sebastian mkazi wa Jimbo la Kawe Jijini Dar na Kada mwaminifu wa Chama cha Mapinduzi ni mwanamke mwenye elimu ya juu lakini amekuwa akiitumia elimu hiyo katika kujitolea kwa shughuli mbalimbali za kukijenga chama hicho kwa muda mrefu sasa.

Kuhusu elimu yake, Maria ana Shahada ya Uzamili katika Utawala wa Biashara kwenye Mashirika ya Umma na Stashahada ya Juu katika Uendeshaji wa Benki na Fedha kutoka Chuo Kikuu cha Mzumbe na Taasisi ya Usimamizi  wa Fedha (Institute of Finance Management).

Pamoja na elimu hiyo, Maria amepata uzoefu kwa kufanyakazi katika  Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kama mchambuzi yakinifu wa biashara ya benki na mifumo ya usalama.

Kwa elimu hiyo ambayo ingeweza kumpa ajira bora kabisa popote ulimwenguni lakini kwa muda mrefu sasa Maria anafanyakazi ya kujitolea katika Chama cha Mapinduzi na jamii kwa ujumla katika kuwawezesha wananchi kiuchumi, kijamii na kisiasa.

Kwa mustakabali huo Maria sasa amechukua fomu ya kutia nia ya kuwania Ubunge wa Jimbo la Kawe ili akawapambanie bungeni wananchi wa jimbo hilo na jina lake limerudi sambamba na watia nia wengine saba wote wanaume mwanamke akiwa peke yake.

Hivyo basi Maria amesema anawaomba wajumbe wa CCM na viongozi wa juu wa chama hicho kulipitisha jina lake kama mgombea pekee ili akawapambanie wananchi wa jimbo hilo katika harakati za kimaendeleo endelevu (Sustanable Development). IMEANDIKWA NA RICHARD BUKOS WA GLOBAL PUBLISHERS.



Prev Post Sekta Binafsi Yahimizwa Kuchangamkia  Fursa Za Kongani Ya Viwanda Pwani
Next Post NMB YAJIZATITI KUSAIDIA WAFUGAJI NA WAVUVI KUPITIA MAONESHO YA NANENANE
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook