Search
Sign In
2Your Cart
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Kamenge: WanaCCM Tuwe Wamoja Kuelekea Uchaguzi

  • 35
Scroll Down To Discover

Mtia nia wa ubunge Jimbo la Missenyi kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Evance Kamenge

Mtia nia wa ubunge Jimbo la Missenyi kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Evance Kamenge, amewapongeza madiwani wa viti maalum waliochaguliwa katika uchaguzi wa ndani wa chama uliofanyika Julai 20, 2025, huku akitoa wito kwa wanachama wote kuendeleza mshikamano na ushirikiano kuelekea uchaguzi mkuu ujao.

Akizungumza na vyombo vya habari, Kamenge alieleza kuwa kipindi hiki cha uchaguzi ni fursa kwa kila mwanachama kunufaika, hivyo ni muhimu kushirikiana kwa pamoja ili kufanikisha maendeleo ya kweli kwa wananchi wa Missenyi.

Aidha, Kamenge aliwatia moyo wale ambao hawakupata nafasi ya kuteuliwa kuwa madiwani wa viti maalum, akiwahimiza kuendelea kuhudumia jamii katika nafasi walizonazo na kusubiri fursa nyingine zijazo.

Kwa sasa, Kamenge anasubiri mchakato wa uteuzi wa wagombea wa ubunge kupitia CCM, huku akisisitiza kuwa endapo atapata nafasi hiyo, atakuwa kiongozi wa vitendo na atawajibika kwa wananchi kwa njia inayoonekana.

“Nina dhamira ya dhati ya kuwatumikia wananchi wa Jimbo la Missenyi vipaumbele vyangu vitakuwa katika uchumi wa uzalishaji na maendeleo ya jamii,” alisema Kamenge.

Kamenge ambaye ni Mchumi na mkulima

ametoa wito kwa wanachama wote wa CCM Missenyi kuendelea kushikamana na kuunga mkono juhudi za chama kupitia Mwenyekiti wa chama hicho Taifa Dkt Samia Suruhu Hassani katika kuleta maendeleo kwa wananchi.

Tufuatilie kupitia YouTube ya Global TV — usisahau ku-like, ku-comment na ku-subscribe ili uendelee kuhabarika kila siku kwa habari mbalimbali zenye ukweli na uhakika.



Prev Post CCM Yatangaza Tarehe ya Kura ya Maoni kwa Ubunge na Udiwani Kufanyika Agosti 4, 2025
Next Post Miaka 25 Ya Vodacom Kuadhimisha Uunganishwaji Kidijitali
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook