Search
Sign In
2 Register
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Wasanii na Wadau wa Urembo Wajitosa Kuchangia Milioni 20 katika CCM Gala Dinner 2025

  • 8
Scroll Down To Discover

Katika kuunga mkono hafla ya CCM Gala Dinner 2025 inayoendelea usiku huu katika Ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar es Salaam, wadau wa sanaa na urembo wamejitokeza kutoa michango ya hali na mali.

Akitangaza kwa niaba ya wasanii, bila kubainisha tanzu wanazotoka, Steve Mengele maarufu kama Nyerere aliahidi kuchangia Sh milioni 10 kwa ajili ya kufanikisha tukio hilo maalum.

Kwa upande wake, mwanamitindo na mdau maarufu wa tasnia ya urembo, Millen Magese, naye alieleza dhamira yake ya kuchangia kiasi sawa cha Sh milioni 10, akisisitiza umuhimu wa mshikamano na mshikikamo katika kuchangia maendeleo kupitia tasnia mbalimbali.

Michango hiyo imeongeza hamasa miongoni mwa wageni waalikwa na wadau wengine waliokusanyika kwenye hafla hiyo ya kifahari, ambayo inalenga kuchangisha fedha kwa ajili ya miradi mbalimbali inayoratibiwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM).



Prev Post CHADEMA Arusha Yawafukuza Wanachama 12 kwa Ukiukaji wa Katiba na Maadili
Next Post CHADEMA Kukata Rufaa Dhidi ya Uamuzi wa Mahakama Kuu Kuhusu Mashahidi wa Siri Kesi ya Lissu – Video
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook