Search
Sign In
2Your Cart
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Rais Samia Afungua Kituo Cha Biashara Na Usafirishaji Afrika Mashariki (EACLC) – Video

  • 12
Scroll Down To Discover

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akisikiliza maelezo kuhusu Kituo cha Biashara na Usafirishaji Afrika Mashariki (EACLC) kilichopo Ubungo Jijini Dar es Salaam tarehe 01 Agosti, 2025.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo Agosti 1, 2025, amefungua rasmi Kituo cha Biashara na Usafirishaji Afrika Mashariki (East African Commercial and Logistics Centre – EACLC) kilichopo eneo la Ubungo, Dar es Salaam.

Kituo hicho kimelenga kuwa kiungo muhimu cha kuimarisha biashara, usafirishaji na usambazaji wa bidhaa ndani ya ukanda wa Afrika Mashariki na Kati, sambamba na kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha kimkakati cha biashara katika kanda.

EACLC kinatarajiwa kuleta mapinduzi makubwa katika sekta ya usafirishaji, ajira, na uwekezaji, huku kikitoa huduma za kisasa kwa wafanyabiashara wa ndani na nje ya nchi.

Rais Dkt. Samia akiwa na Viongozi pamoja na Wananchi mbalimbali waliohudhuria hafla ya ufunguzi wa Kituo cha Biashara na Usafirishaji Afrika Mashariki (EACLC).
Rais Samia akiwa kwenye ufunguzi wa Kituo cha Biashara na Usafirishaji Afrika Mashariki (EACLC).

Rais  Samia akitembelea maduka yaliyopo katika Kituo cha Biashara na Usafirishaji Afrika Mashariki (EACLC) kilichopo Ubungo Jijini Dar es Salaam tarehe 01 Agosti, 2025.

 



Prev Post YANGA KUMPA KAZI YA UKOCHA KIJANA WA MIAKA 35 WAMEPATIA..? UKWELI UNAOPASWA KUJUA HUU HAPA…
Next Post Kamanda wa Polisi Mtwara Afunguka Kuhusu Tukio la Ebitoke
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook