Search
Sign In
2Your Cart
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Humphrey Polepole Ajiuzulu Ubalozi Ampongeza Rais Samia Kwa Fursa

  • 36
Scroll Down To Discover

Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Cuba, Humphrey Polepole, amemuandikia barua Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, akitangaza kujiuzulu rasmi nafasi yake ya uwakilishi wa taifa hilo katika nchi ya Cuba, ukanda wa Karibe, Amerika ya Kati, pamoja na mataifa rafiki ya Colombia, Venezuela na Guyana.

Historia Fupi ya Utumishi wa Polepole

Humphrey Polepole amewahi kushika nafasi mbalimbali ndani ya Serikali ya Tanzania, zikiwemo:

Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (Novemba 2020 – Machi 2022).

Balozi wa Tanzania nchini Malawi (Machi 2022 – Aprili 2023).

Balozi wa Tanzania nchini Cuba (Aprili 2023 – Julai 2025).

Polepole pia alijulikana kwa muda mrefu kama mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama hicho, akiwa mmoja wa watetezi wakubwa wa maadili ya chama na utawala bora.



Prev Post Makalla: Hakuna Mtia Nia Aliyeenguliwa CCM, Mchakato Bado Unaendelea – Video
Next Post Majaliwa Amwakilisha Rais Dkt. Samia Ibada Ya Kuwekwa Wakfu Askofu Mteule Dkt. Daniel Mono
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook