Search
Sign In
2Your Cart
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Equatorial Guinea: Baltasar Engonga Atupwa Jela Miaka 18 kwa Ubadhirifu

  • 8
Scroll Down To Discover

Malabo, Julai 2, 2025 – Mahakama ya Juu ya Equatorial Guinea imemhukumu aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Kitaifa la Uchunguzi wa Fedha, Baltasar Engonga, kifungo cha miaka 18 jela baada ya kupatikana na hatia ya makosa kadhaa ya kifisadi na matumizi mabaya ya madaraka.

Kwa mujibu wa taarifa rasmi kutoka Mahakama ya Malabo, Engonga amekutwa na hatia ya ubadhirifu wa zaidi ya Faranga bilioni 1, ambapo Faranga milioni 910 alizitia kibindoni kwa matumizi binafsi, hasa kwa anasa, wanawake na maisha ya kifahari yaliyo nje ya uwezo wa mshahara wake wa umma.

Mbali na tuhuma hizo, Engonga alihusishwa na:

Ubadhirifu wa mali ya umma

Uhusiano wa kingono kazini kinyume na maadili

Kushirikiana na maafisa wa zamani kuendesha mtandao wa kifisadi

Hata hivyo, Mahakama imebainisha kuwa hukumu hiyo haihusiani moja kwa moja na kashfa kubwa ya mwaka 2024 iliyohusisha video zaidi ya 400 za faragha zilizovuja na kuzua taharuki kimataifa.

Engonga, ambaye kwa miaka mingi alihusishwa na ngazi za juu za mamlaka nchini humo, amekuwa gumzo la kitaifa tangu ripoti za awali za uchunguzi zilipoanza kusambaa mwaka 2023. Hukumu hiyo imepokelewa kwa hisia tofauti miongoni mwa wananchi na wachambuzi wa kisiasa, huku wengi wakitaka hatua zaidi dhidi ya “mtandao mkubwa wa kifisadi” ulioibuliwa na kesi hiyo.

BABA wa MSANII WEMA wa SHILINGI ALIYEFARIKI ASHTUA – “NINA SHAKA na KIFO cha MWANANGU-SIKUONA MAITI”



Prev Post PITIA VICHWA VYA HABARI KATIKA MAGAZETI YA LEO JUNI 25, 2025
Next Post TAMASHA LA SABASABA KUINUA UCHUMI WA UBUNIFU NA KUWEZESHA WASANII NA FAMILIA
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook