Search
Sign In
2Your Cart
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Furaha Dominic Aliyekubalika na Wajumbe Kawe Airudia Tena Kawe Yake

  • 43
Scroll Down To Discover

Furaha Dominic alipokuwa akizungumza na Global Tv baada ya kuchukua fomu ya kutia nia ya Kugombea Jimbo la Kawe.

Kama kuna kitu kilichowaumiza watu wa Jimbo la Kawe haswa wajumbe waliompitisha kugombea katika Uchaguzi Mkuu wa 2020 ni kumchagua kwa kura za kutosha kuwaongoza mtia nia ya Ubunge Kijana Msomi na Kada wa Chama cha Mapinduzi, Furaha Dominic ambaye hata hivyo jina lake lilikatwa kwa sababu ambazo hazikuwekwa wazi.

Furaha akizungumza na mtia nia mwenzake wa Jimbo la Kawe John Warioba Mwita baada ya wote kuchukua fomu.

Katika kuonekana kutaka kuwarejeshea furaha yao wajumbe hao na wakazi wa Jimbo la Kawe kwa ujumla kada huyo wa Chama cha Mapinduzi CCM mwaka huu amerejea tena na kutia nia ya kuligombea jimbo hilo lililokuwa likishikiliwa na Mchungaji Josephat Gwajima aliyewekwa nafasi hiyo akiwa nafasi ya tatu katika kura za maoni ya wajumbe baada ya jina la Furaha Dominic lililokuwa namba moja kukatwa.

Furaha akizungumza na Mbunge wa Jimbo la Kinondoni aliyemaliza muda wake na kutia ya kuendelea, Abbas Tarimba. Katikati ni Msaidizi wa Furaha aliyefahamika kwa jina la Bildad.

Mwanahabari wetu alimshuhudia Furaha akirejesha fomu ya kutia nia ya kugombea jimbo hilo katika Ofisi za CCM Wilaya ya Kinondoni huku akionekana mwenye furaha tele na kuwachangamkia watia nia wenzake huenda ni baada ya kuwachungulia anaopambana nao.

Watia nia wakibadilishana mawazo.

Furaha ni kama anaurejea mtihani ambao alishawahi kuufaulu. Watia nia wengine wanaendelea kwenda kuchukua na kurudisha fomu za kuligombea jimbo hilo.  HABARI/PICHA :RICHARD BUKOS, GPL



Prev Post Kazi ipo! Hamisi Slim wa Equator Grill Achukua Fomu Kuwania Udiwani
Next Post Pruuu Mpaka Michenzani!
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook