
Mganga Mfawidhi wa Wilaya ya Arusha, Saidi Salimu, amepata ajali ya gari akiwa na gari yake ndogo aina ya Benz lenye namba za usajili T782 EHP katika Barabara ya East Africa, maeneo ya Karavati, baada ya kugongwa na lori aina ya Fuso lenye namba za usajili T224 BRS ambalo lilipata hitilafu ya breki.
Kwa mujibu wa mashuhuda, mganga huyo aliokolewa akiwa amevunjika miguu yote miwili baada ya kubanwa ndani ya gari, na mara moja alikimbizwa katika Kituo cha Afya Murieti kwa matibabu.
Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!