Search
Sign In
2Your Cart
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Familia Yahuzunishwa Kupotea Kwa Mama Wa Watoto Wanne

  • 34
Scroll Down To Discover

Happy Peter ni mama wa watoto wanne, alikuwa anaishi na mume wake katika maeneo ya Boko Timiza, Kibaha, mkoani Pwani. Alijulikana kwa tabia yake ya upendo, uchapakazi, na kujitolea kwa familia yake. Hata hivyo, tarehe 4 Mei 2025, maisha ya familia yake yalibadilika ghafla.

Happy aliondoka nyumbani kwake kama kawaida, lakini hakurejea tena. Mume wake na watoto walipata wasiwasi mkubwa baada ya kutomwona kwa masaa kadhaa. Jioni ilipofika bila taarifa yoyote kutoka kwake, familia ilianza kuwasiliana na ndugu, majirani, na marafiki kwa matumaini ya kupata taarifa yoyote kuhusu alipo.

Kwa bahati mbaya, hakuna aliyekuwa na habari kuhusu alikoelekea. Juhudi za kumtafuta zilianza mara moja, huku familia ikifika katika vituo vya polisi kutoa taarifa ya kupotea kwake. Polisi walipokea taarifa hiyo na kufungua jalada la tukio kwa kumbukumbu namba KBA/RB/2642/2025.

Happy ameacha watoto wanne ambao sasa wanakosa upendo na msaada wa mama yao. Familia yake inatoa wito kwa yeyote atakayemuona au kuwa na taarifa zozote kuhusu alipo, kuwasiliana kupitia namba zifuatazo:

📞 0719 379 188
📞 0684 177 888

Vilevile, wananchi wanahimizwa kutoa taarifa katika kituo chochote cha polisi kilicho karibu. Familia ya Happy Peter inaomba msaada wa umma katika juhudi za kumtafuta mama huyu ambaye kupotea kwake kumewaacha watoto wake katika hali ya huzuni na sintofahamu kubwa.

 



Prev Post Papa Leo wa XIV azungumza kwa simu na Rais Zelensky
Next Post Bunge Lapitisha Bajeti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ya Trilioni 2.4
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook