Search
Sign In
2 Register
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Rais Samia Ashiriki Kongamano la Amani Kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 – Video

  • 1
Scroll Down To Discover

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na viongozi mbalimbali pamoja na wageni waalikwa waliohudhuria Kongamano la Amani kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2025 lililoandaliwa na Umoja wa Maimamu Tanzania (UMATA) katika ukumbi wa Diamond Jubilee Jijini Dar es Salaam tarehe 24 Agosti, 2025.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo Jumapili, Agosti 24, 2025, ameshiriki Kongamano la Amani kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2025 lililofanyika katika Ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam.

Kongamano hilo limewaleta pamoja viongozi wa dini, vyama vya siasa, taasisi za kiraia, vijana na wadau mbalimbali wa amani kwa lengo la kuhamasisha mshikamano wa kitaifa na kudumisha utulivu wa nchi wakati wa kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba 2025.

Katika hotuba yake, Rais Samia amesisitiza dhamira ya Serikali na vyombo vya usalama kuhakikisha uchaguzi unakuwa huru, wa haki na wa amani, akiwataka Watanzania kuendelea kudumisha mshikamano na mshikikiano bila kujali tofauti za kisiasa.

Matukio mbalimbali kwenye Kongamano la Amani kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2025 lililoandaliwa na Umoja wa Maimamu Tanzania (UMATA) katika ukumbi wa Diamond Jubilee Jijini Dar es Salaam tarehe 24 Agosti, 2025.
Rais Samia akiombewa dua na watoto yatima wa Kituo cha Watoto Yatima Mburahati mara baada ya kuwasili katika ukumbi wa Diamond Jubilee Jijini Dar es Salaam tarehe 24 Agosti, 2025 kwa ajili ya kushiriki kwenye Kongamano la Amani kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2025 lililoandaliwa na Umoja wa Maimamu Tanzania (UMATA).
Rais Samia akisalimiana na viongozi mbalimbali mara baada ya kuwasili katika ukumbi wa Diamond Jubilee Jijini Dar es Salaam tarehe 24 Agosti, 2025 kwa ajili ya kushiriki kwenye Kongamano la Amani kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2025 lililoandaliwa na Umoja wa Maimamu Tanzania (UMATA).



Prev Post Mashirika ya Umma Yatambuliwa Kwa Ufanisi
Next Post TRAMPA Yafika Gereza la Ukonga Kuonesha Matendo ya Huruma kwa Wafungwa
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook