
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Ridhiwani Kikwete, ametembelea banda la Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) katika Kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi 2025 yanayoendelea mkoani Singida ambapo amekutana na kuongea na wafanyakazi wenye mahitaji maalumu ambao ni waajiriwa wa WCF.
Watumishi hao walimueleza Kikwete namna WCF inavyowajumuisha kikamilifu katika kila hatua na matukio yote yanayohusisha wafanyakazi na kuwawezesha kwa kuwapatia vifaa wezeshi vinavyowarahisishia kutekeleza majukumu yao ya kila siku.
Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!