MAGAZETI ya Leo Jumatatu 28 April 2025
Sare ya bila kufungana dhidi ya Stellenbosch ugenini kwenye Uwanja wa Moses Mabhida, Durban Afrika Kusini leo Aprili 27, 2025 imeivusha Simba kwenda hatua ya fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika ikibebwa na ushindi wa bao 1-0 ilioupata katika mechi ya kwanza nyumbani Jumapili iliyopita.
Stellenbosch ambao katika mechi nyingi za mashindano hayo wamekuwa wakicheza kwa kutegemea mashambulizi ya kushtukiza, katika mchezo wa leo walionekana kuingia tofauti ambapo walimiliki mpira na kushambulia kwa muda mrefu lakini safu ya ulinzi ya Simba ilikuwa imara kuondosha hatari ambazo ilielekezewa.
Katika mchezo huo, kulikuwa na matukio mawili makubwa ambayo yalimlazimisha refa Mohamed Maarouf Eid Mansour kutoka Misri kwenda kutazama marejeo kupitia teknolojia ya video ya usaidizi kwa marefa (VAR) na kulazimika kubadilisha uamuzi wa awali.
Tukio la kwanza lilikuwa ni dakika ya 11 ambapo refa huyo aliizawadia Simba mkwaju wa penalti baada ya awali kudhani Kibu Denis aliangushwa katika eneo la hatari lakini baada ya kulitazama upya tukio hilo, alibatilisha uamuzi wake.
La pili lilikuwa katika dakika ya 78 ambapo Genino Palace aliifungia bao Stellenbosch lakini mwamuzi Mansour alilibatilisha baada ya kujiridhisha kuwa kulikuwa na tukio la kuotea wakati bao hilo linatengenezwa.
Licha ya Stellenbosch kuongeza kasi ya mashambulizi, Simba ilionyesha uimara katika kujilinda na ikawanyima wapinzani wao fursa ya kufunga bao hadi filimbi ya mwisho ilipopulizwa.
Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!