Baada ya dabi ya Kariakoo kati ya Simba na Yanga iliyopigwa jana Jumapili kwenye Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo jijini Dar es Salaam kumalizika kwa sare ya mabao 2-2, mpiga picha maarufu nchini, Rommy3D, ameweka wazi rangi zake halisi.
Rommy amevunja ukimya na kutangaza rasmi kuwa yeye ni shabiki lialia wa klabu ya Yanga, huku akimwaga sifa kwa nyota wanaofanya kazi nzuri ndani ya kikosi hicho cha mabingwa watetezi.
Katika maelezo yake yaliyojaa mahaba kwa klabu hiyo ya Jangwani, Rommy amebainisha kuwa ubora wa Yanga kwa sasa unachagizwa na nguzo imara alizozitaja kuwa ni Ibrahim Hamad ‘Bacca’, kiungo fundi Salum Abubakar ‘Sure Boy’, pamoja na kipa stadi Djigui Diarra.
Kwa mujibu wa mpiga picha huyo, mchango wa watatu hao uwanjani umekuwa chimbuko la furaha yake kama shabiki, kutokana na kiwango chao cha hali ya juu na utulivu wanapokuwa na mpira.
The post ROMMY3D AWATAJA BACCA, DIARRA KAMA NGUZO MUHIMU YANGA appeared first on Soka La Bongo.






Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!