Search
Sign In
2Your Cart
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Watanzania na Wanajumuiya ya Afrika Mashariki Wahimizwa Kudumisha Amani

  • 21
Scroll Down To Discover

Mchungaji Haron Muturi kutoka nchini Kenya akisalimiana na Mtumishi Victor Chihimba mara baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam kwaajili ya kushiriki Wiki ya Uamsho na Kuliombea Taifa mara baada ya kupokea mualiko na kwaya ya Gethsemane Group Kinondoni (GGK) kutoka Kanisa la Wadventista Wasabato Kinondoni Jijini Dar es Salaam.

Dar es Salaam 24 Aprili 2025: Watanzania na Wanajumuiya ya Afrika Mashariki wametakiwa kuendelea kudumisha amani na hasa kipindi hiki ambacho Taifa la Tanzania linaelekea katika Uchaguzi Mkuu unaotarajia kufanyika Oktoba mwaka huu.
Kauli hiyo imetolewa na  Mchungaji Patrick  Muthee kutoka nchini Kenya ambao wapo nchini Tanzania kwa mwaliko  wa Kwaya ya Gethsemane Group Kinondoni (GGK) kutokea Kanisa  la Wadventista Wasabato Kinondoni Jijini Dar es Salaam  pamoja na uongozi wa kanisa  ambapo wameandaa Wiki ya maombi yakiwemo ya kuliombea Taifa letu la Tanzania amani,upendo na mshikamano.

Wachungaji kutoka nchini Kenya, Mchungaji Haron Muturi pamoja na Mchungaji Patrick Muthee wakipokelewa na wanakwaya ya Gethsemane Group Kinondoni (GGK) kutoka Kanisa la Wadventista Wasabato Kinondoni Jijini Dar es Salaam..

“Tumekuja nchini Tanzania kuungana na ndugu zetu wa Kwaya ya Gethsemane pamoja na Kanisa Group Kinondoni (GGK)ambapo wameandaa wiki ya maombi mbalimbali ya kuliombea Taifa na kwa wakati huu kuomba amani,Umoja na mshikamano ni kipaumbele chetu kwani tunatambua Watanzania watakuwa na uchaguzi Mkuu mwaka huu.Hivyo tunawaombea wawe na amani.”

Mchungaji Patrick Muthee kutoka nchini Kenya akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuwasili.

Pia  Mchungaji Mwangi amesema Tanzania na Kenya wamekuwa na mahusiano ya karibu na undugu wao umekuwepo tangu wakati wanamfukuza mkoloni na kupata uhuru na hiyo imeipatia Kanisa kipaumbele kupeleka injili pamoja na kanisa la Waadventista Wasabato Kinondoni kinondoni na kiongozi wa jumuiya ya Afrika.

Mchungaji Haron Muturi kutoka nchini Kenya akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam kwaajili ya kushiriki Wiki ya Uamsho na Kuliombea Taifa mara baada ya kupokea mualiko na kwaya ya Gethsemane Group Kinondoni (GGK) kutoka Kanisa la Wadventista Wasabato Kinondoni Jijini Dar es Salaam.



Prev Post AMERICAN ROULETTE MCHEZO RAHISI WA KUBASHIRI GURUDUMU LA NAMBA….
Next Post MAGAZETI ya Leo Jumamosi 26 April 2025
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook