Search
Sign In
2 Register
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Mahakama Yakataa Ombi la Ahirisho la Kesi ya Uhaini ya Tundu Lissu

  • 2
Scroll Down To Discover

Mahakama Kuu, Masjala Ndogo ya Dar es Salaam, imekataa ombi lililotolewa na upande wa Jamhuri la kutaka kuahirishwa kwa siku 14 kwa kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu, kwa kile walichoeleza kuwa ni sababu za kiusalama.

Ombi hilo liliwasilishwa leo Jumatatu na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Tawab Issa, wakati kesi hiyo ilipoitwa kwa ajili ya kusikilizwa.

Baada ya kusikiliza hoja hizo, jopo la majaji watatu likiongozwa na Jaji Dunstan Nduguru lilikataa ombi hilo na kueleza kuwa hakuna sababu za msingi za kuahirisha kesi hiyo, hivyo kesi itaendelea kama ilivyopangwa Jumatano, Novemba 12, 2025, saa tatu kamili asubuhi.



Prev Post Rais Samia Ateua Wabunge Sita Wapya wa Bunge la 13 – Video
Next Post PITIA VICHWA VYA HABARI KATIKA MAGAZETI YA LEO NOBEMBA 11, 2025
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook