Search
Sign In
2Your Cart
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Rais Samia Atuma Salamu za Rambirambi Kufuatia Kifo cha Baba Mtakatifu Francisko

  • 16
Scroll Down To Discover

Rais Samia Suluhu Hassan, ameungana na viongozi wengine duniani kutuma salamu za pole kufuatia kifo cha Kiongozi wa Kanisa katoliki Duniani, Papa Francis.

Kupitia akaunti yake ya Instagram, Rais Samia ameandika:

“Nimesikitishwa na taarifa ya kifo cha Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani, Papa Francisko.

“Katika kipindi chote cha miaka 12 akiwa Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani, Papa Francisko ameishi maisha yake kama mwalimu na kiongozi aliyefundisha na kuhimiza ustawi na maendeleo ya watu pamoja na kudumisha amani.

“Kwa niaba ya Serikali na Wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ninatuma salamu za pole kwa waumini wote wa Kanisa Katoliki hapa nchini na duniani kote.

“Mwenyezi Mungu ailaze roho yake mahali pema Peponi. Amina.”

🔴 Tufuatilie kupitia YouTube ya Global TV, like, comment ili kuendelea kuhabarika kila siku kwa habari mbalimbali zenye ukweli na uhakika.



Prev Post Nguvu za mungu wa Kigiriki Zeus Unazipata Meridianbet Kasino
Next Post MAGAZETI ya Leo Jumanne 22 April 2025
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook