Search
Sign In
2 Register
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Rais Ruto Aongoza Viongozi Kuuaga Mwili wa Raila Odinga Kasarani

  • 11
Scroll Down To Discover

Rais Ruto aongoza viongozi kuuaga mwili wa Raila

Shughuli ya kuuaga mwili wa aliyekuwa Waziri Mkuu wa zamani wa Kenya, Raila Amolo Odinga, imeanza leo katika Uwanja wa Kasarani, jijini Nairobi, ambapo maelfu ya wananchi na viongozi mbalimbali wamejitokeza kutoa heshima zao za mwisho.

Miongoni mwa viongozi waliohudhuria mapema ni Rais wa Kenya, Dkt. William Ruto, ambaye ameongoza viongozi wa serikali, wanasiasa, na mabalozi katika kuuaga mwili wa kiongozi huyo mkongwe aliyekuwa nguzo muhimu katika siasa na harakati za demokrasia nchini humo.

Rais mstaafu wa Kenya Uhuru Kenyatta ampa heshima zake za mwisho Raila

Pia, aliyekuwa Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta, pamoja na viongozi wa vyama vya kisiasa, wabunge, na viongozi wa kidini wameonekana wakiwasili Kasarani kwa ajili ya kushiriki shughuli hiyo ya kitaifa.

Uwanja wa Kasarani umefurika wananchi waliovaa mavazi yenye picha na rangi zinazohusishwa na chama cha ODM, wakipaza nyimbo za kumkumbuka Raila kwa mchango wake mkubwa katika harakati za haki na usawa.

Ratiba ya mazishi inatarajiwa kuendelea kwa siku kadhaa, huku mwili wa Raila ukitarajiwa kusafirishwa hadi kijijini kwake Bondo, Kaunti ya Siaya, kwa ajili ya maziko yatakayofanyika mwishoni mwa wiki hii.

Mkuu wa mawaziri wa Kenya Musalia Mudavadi akiaga mwili wa Raila
Naibu rais Kindiki Kithure.



Prev Post Rc Chalamila Atembelea  Na  Kukagua Miundombinu  Ya Tanesco Dsm
Next Post PITIA VICHWA VYA HABARI KATIKA MAGAZETI YA LEO OKTOBA 17, 2025
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook