Search
Sign In
2Your Cart
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, Gissima Nyamohanga Afariki Dunia Kwa Ajali

  • 12
Scroll Down To Discover

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), Mhandisi Gissima Nyamohanga amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika ajali ya gari iliyotokea Bunda mkoani Mara.

Taarifa za kifo chake zimethibitishwa na Meneja wa Tanesco Mkoa wa Mara na kueleza kuwa mwili wake umehifadhiwa katika Hospitali ya DDH wilayani humo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, pia amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kueleza kuwa atatoa taarifa kamili baadaye.

Chanzo cha ajali hiyo iliyosababisha pia kifo cha dereva wa mkurugenzi huyo, kinaelezwa kuwa ni dereva wa Toyota Land Cruiser, gari alilokuwemo mkurugenzi huyo, kujaribu kumkwepa mwendesha baiskeli na kwenda kugongana na lori.



Prev Post MAGAZETI ya Leo Jumapili 13 April 2025
Next Post Trump Aondoa ushuru kwa simu za mkononi, kompyuta, na vifaa vingine vya kielektroniki
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook