MAGAZETI ya Leo Ijumaa 04 April 2025
Tanzania imeanguka kwa nafasi moja katika chati ya viwango vya ubora wa soka vya Shirikisho la Mpira wa Miguu duniani (FIFA) kwa mujibu wa viwango vilivyotolewa leo, Aprili 3, 2025.
Kwa sasa Tanzania ipo katika nafasi ya 107 ikiwa na pointi 1196.04 tofauti na viwango vilivyopita vya Desemba 19, 2024 ilipokuwa nafasi ya 106 ikiwa na pointi 1199.
Anguko hilo linaonekana kuchangiwa kwa kiasi kikubwa na timu ya taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ kupoteza mechi ya kuwania kufuzu Fainali za Kombe la Dunia dhidi ya Morocco, Machi 25 mwaka huu kwa mabao 2-0.
Maumivu ya kuanguka katika viwango vya ubora vya FIFA hayajaikuta Tanzania pekee bali pia nchi za Uganda, Kenya, Sudan, Rwanda, Burundi, Ethiopia na Djibouti ambazo pia ni nchi wanachama wa Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu Afrika Mashariki na Kati (CECAFA).
Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!