Search
Sign In
2Your Cart
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Rais Samia Apokea Tuzo ya Heshima ya ‘Power of 100 Women’

  • 31
Scroll Down To Discover

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea Tuzo Maalum ya ‘Power of 100 Women Award kutoka kwa Uongozi wa Access Bank Group kutoka kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Access Tanzania Ndugu Protase Ishengoma Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Julai, 2025. Tuzo hii ambayo hutolewa kila baada ya miaka mitano inalenga kutambua na kusherehekea wanawake wa Kiafrika wanaotoa michango ya mageuzi kwa mataifa na jamii zao, kuhamasisha na kuhimiza kizazi kijacho cha viongozi Wanawake katika bara zima la Afrika. Pia kupaza sauti za Wanawake katika kuleta maendeleo endelevu ya Kiuchumi na kijamii barani Afrika.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan leo Julai 8, 2025 amepokea Tuzo Maalum ya Heshima ya ‘Power of 100 Women’ kutoka kwa Uongozi wa Access Bank Group, ikiwa ni kutambua mchango wake mkubwa katika kuleta mageuzi ya kijamii na kiuchumi barani Afrika, hususan katika kuhamasisha ushiriki wa wanawake katika uongozi.

Tukio hilo limefanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, ambapo tuzo hiyo ilikabidhiwa rasmi kwa Rais Samia na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Access Tanzania, Ndugu Protase Ishengoma, kwa niaba ya uongozi mzima wa Access Bank Group.

Tuzo ya Power of 100 Women hutolewa kila baada ya miaka mitano kwa lengo la kutambua, kusherehekea na kutia moyo wanawake wa Kiafrika wanaoleta mabadiliko makubwa katika mataifa yao, na kuchochea kizazi kipya cha wanawake viongozi barani Afrika. 



Prev Post Said Mrisho: Nilitobolewa Macho, Nikachomwa Visu, Lakini Haki Yangu Haijatimia – Video
Next Post Waziri Mkuu Majaliwa Afungua Kikao Kazi Cha TRA, Ahimiza Tathmini Na Uboreshaji Wa Utendaji
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook