Search
Sign In
2 Register
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Rais Mwinyi aungana na Waislamu Maulid Kitaifa Zanzibar

  • 4
Scroll Down To Discover

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Alhaj Dkt. Hussein Ali Mwinyi, usiku wa Septemba 4, 2025, ameungana na maelfu ya waumini wa Kiislamu katika Maulid Makuu ya Kitaifa ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (S.A.W), yaliyofanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja, Zanzibar.

Sherehe hizo ziliambatana na qaswida, dua, na mihadhara ya kidini iliyoeleza historia na mafunzo ya Mtume Muhammad (S.A.W), yakisisitiza mshikamano, amani na mshikamo wa kijamii.

Dkt. Mwinyi alisisitiza umuhimu wa kufuata maadili na mwenendo wa Mtume (S.A.W) katika maisha ya kila siku, akiwataka wananchi kuendeleza mshikamano wa kidini na kitaifa kwa ajili ya maendeleo ya Zanzibar na Tanzania kwa ujumla.



Prev Post PITIA VICHWA VYA HABARI KATIKA MAGAZETI YA LEO SEPTEMBA 05, 2025
Next Post CHAUMMA Jimbo la Segerea Kwazidi Kuwaka
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook