Search
Sign In
2Your Cart
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Ruto Atangaza Hatua Kali Dhidi ya Maandamano ‘Inatosha!’

  • 33
Scroll Down To Discover

Rais wa Kenya, William Ruto

Rais wa Kenya, William Ruto, ameapa kuchukua hatua kali kuhakikisha kuwa amani na utulivu vinarejea nchini, akisema yuko tayari kutumia mbinu zozote zinazohitajika kukomesha wimbi la maandamano ya hivi karibuni.

Akizungumza kwa hisia kali katika hafla ya uzinduzi wa makazi ya polisi jijini Nairobi, Rais Ruto alisema:

“Inatosha! Hatuwezi kuruhusu hali hii iendelee. Tutatumia njia zozote kuhakikisha nchi inabaki salama na yenye utulivu.”

Kauli hiyo imekuja baada ya maandamano makubwa ya vijana – maarufu kama ‘Gen Z’ yaliyoanza mwezi Juni 2024, kupinga nyongeza ya kodi, lakini baadaye kugeuka kuwa wito wa mabadiliko ya kiutawala, ikiwa ni pamoja na:

Ruto ajiuzulu

Kukomeshwa kwa ukatili wa polisi

Kupinga ufisadi na matumizi mabaya ya rasilimali

Rais Ruto kwa mara ya kwanza amejibu kwa ukali maandamano hayo, akiwatuhumu wanasiasa wa upinzani kuhusika na kupanga mikakati ya kumng’oa madarakani:

“Ni viongozi wanaowafadhili vijana kutekeleza vitendo hivyo. Tunawafuatilia!”

Aliwaonya kuwa wanaotaka urais wa Kenya wasijifiche nyuma ya maandamano, bali wakutane naye 2027, wakati wa uchaguzi mkuu ujao.

NAIBU WAZIRI MKUU BITEKO APASUA UKWELI – “KAWAIDA KUGAWANYIKA WAKATI wa UCHAGUZI -HATUWEZI KUFANANA”



Prev Post TZS BILIONI 1.5 ZIPO MEZANI, JIUNGE NA LUCKY RUSH TOURNAMENT YA MERIDIANBET LEO
Next Post DCEA Yatangaza Vita Dhidi ya Usafirishaji wa Dawa za Kulevya Kupitia Maiti – Video
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook