Search
Sign In
2Your Cart
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

CCM Yatangaza Idadi ya Wagombea Ubunge, Zaidi ya 4,000 Wajitokeza – Video

  • 9
Scroll Down To Discover

Dar es Salaam, Julai 3, 2025 – Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC), Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), CPA Amos Makalla, ametangaza kuwa jumla ya wanachama 5,475 wamechukua fomu kuwania nafasi za Ubunge na Ujumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar katika uchaguzi mkuu ujao wa 2025.

Akizungumza leo katika Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam, Makalla amesema kuwa zoezi hilo la kuchukua na kurejesha fomu lilihitimishwa rasmi hapo jana, Julai 2, 2025.

Kwa mujibu wa Makalla, kwa nafasi ya ubunge katika majimbo yote 272 ya uchaguzi nchini:

Watia nia kutoka Tanzania Bara ni 3,585

Watia nia kutoka Zanzibar ni 524

Wanawake waliojitokeza kugombea ni 263

Aidha, kwa upande wa Ujumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, jumla ya wagombea 503 walichukua fomu.

Makalla ameeleza kuwa idadi hiyo inaonesha mwitikio mkubwa wa wanachama wa CCM katika kushiriki kuwania nafasi za uongozi ndani ya mfumo wa kidemokrasia wa chama, na kwamba hatua inayofuata ni mchakato wa uchujaji utakaoanza rasmi kesho.

“Tunajivunia kuona wanachama wetu wengi wamejitokeza. Huu ni ushahidi wa imani kubwa waliyonayo kwa chama na mfumo wake wa kiuongozi,” amesema Makalla.



Prev Post Twende Butiama 2025 Yaanza Rasmi Kutoka Dar Es Salaam
Next Post Serikali Itaendelea Kuimarisha Mazingira Ya Ufanyaji Biashara-Majaliwa
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook