Search
Sign In
2Your Cart
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Wizara ya Katiba na Sheria Yakamilisha Kampeni ya Msaada wa Kisheria Katika Mikoa 25 – Video

  • 17
Scroll Down To Discover

Waziri wa Katiba na Sheria nchini Tanzania, Dkt. Damas Ndumbaro

Waziri wa Katiba na Sheria nchini Tanzania, Dkt. Damas Ndumbaro, ameeleza kuwa wizara yake inaendelea na uratibu na utekelezaji wa Kampeni ya Kitaifa ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia, ambapo hadi sasa kampeni hiyo imetekelezwa katika mikoa 25 ya Tanzania Bara, huku Dar es Salaam ikiwa ndiyo mkoa pekee uliosalia.

Akiwasilisha hotuba ya bajeti ya Wizara ya Katiba na Sheria kwa mwaka wa fedha 2025/26 leo, Jumatano, Aprili 30, 2025, bungeni jijini Dodoma, Waziri Ndumbaro amelieleza Bunge kuwa kufikia mwezi Juni mwaka huu, kampeni hiyo itaanza rasmi katika Mkoa wa Dar es Salaam ili kukamilisha utekelezaji wake katika mikoa yote ya Tanzania Bara.

Katika hatua nyingine, Waziri Ndumbaro amezungumzia pia utekelezaji wa kampeni hiyo Visiwani Zanzibar, akieleza kuwa tayari imefanyika katika mikoa ya Kaskazini Pemba, Mjini Magharibi na Kaskazini Unguja, na kwa sasa inatekelezwa katika mikoa ya Kusini Pemba na Kusini Unguja, ambapo inatarajiwa kukamilika mwezi Mei mwaka huu.



Prev Post Mataifa 9 Yenye Uwezo Mkubwa wa Silaha Hatari za Nyuklia
Next Post Meridianbet Yakupa Nafasi Ya Kishua – Shinda Simu Mpya Ya Samsung A25!
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook