Search
Sign In
2 Register
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Machumu Ateuliwa Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Tido Mshauri wa Rais – Video

  • 15
Scroll Down To Discover

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amefanya mabadiliko ya uongozi katika Kitengo cha Mawasiliano Ikulu kwa kufanya uteuzi mpya wa viongozi wawili wapya.

Katika taarifa iliyotolewa tarehe 19 Novemba 2025 na Ofisi ya Katibu Mkuu Kiongozi, kupitia Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Moses Mpogole Kusiluka, Rais Samia amemteua Bakari Steven Machumu kuwa Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu.

Machumu, ambaye ni aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Mwananchi Communications Limited (MCL), anachukua nafasi ya Sharifa Bakari Nyanga, ambaye amepangiwa majukumu mengine serikalini.

Katika hatua nyingine, Rais Samia pia amemteua Tido Mhando, mwanahabari mkongwe na mmoja wa viongozi wenye uzoefu mkubwa katika tasnia ya habari, kuwa Mshauri wa Rais, Habari na Mawasiliano.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa viongozi hao wataapishwa na kuanza kutekeleza majukumu yao mapya muda mfupi ujao, kulingana na utaratibu wa Ikulu.



Prev Post PITIA VICHWA VYA HABARI KATIKA MAGAZETI YA LEO NOVEMBA 19, 2025
Next Post Rais Samia Amteua Lazaro Nyalandu Kuwa Balozi
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook