Search
Sign In
2Your Cart
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

MAGAZETI ya Leo Jumatatu 14 April 2025

  • 21
Scroll Down To Discover

MAGAZETI ya Leo Jumatatu 14 April 2025

Tanzania iko mbioni kuacha kuagiza vilipuzi na baruti kutoka nje ya nchi. Kila mwaka Tanzania inaagiza vilipuzi milioni 10 na tani 26,000 za baruti kutoka nje.

Waziri wa Madini, Anthony Mavunde amesema nchi iko mbioni kuachana na uagizaji wa bidhaa hiyo kutoka nje ya nchi kutokana na uzalishwaji wa zana hizo muhimu katika sekta ya madini.

Amesema Kiwanda cha Solar Nitrochemicals Limited kilichozinduliwa Jumapili, Aprili 13, 2025 kitakuwa na uwezo wa kuzalisha bidhaa hiyo zaidi ya mahitaji.

Akizindua kiwanda hicho kilichogharimu Sh19 bilioni, Waziri Mavunde amesema kitazalisha tani 22,000 za baruti na vilipuzi milioni 15 kwa mwaka.

“Tunaelekea kuacha kuagiza vilipuzi na baruti kutoka nje,” amesema Mavunde wakati wa uzinduzi wa kiwanda hicho kilichopo eneo la Visegese, Kisarawe mkoani Pwani.

Amesema kiwanda hicho ni cha kwanza kuzalisha kiwango kikubwa cha baruti na vilipuzi nchini na kwamba, uzalishaji huo utaongeza pato la Taifa kupitia sekta ya madini.



Prev Post Zaidi Ya Wanachama 50 Wa ACT Wazalendo Lindi Watimkia CCM, Wafichua Sababu Nzito
Next Post Mstaafu Kikwete Awasilisha Ujumbe Maalum Kwa Waziri wa Nchi ya Guinea ya Ikweta
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook