Search
Sign In
2 Register
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

NMB YAINGIA AMAMU MPYA YA UBORA WA HUDUMA KWA WATEJA

  • 27
Scroll Down To Discover

Benki ya NMB imekamilisha uhamishaji wa shughuli zake kwenda katika Mfumo Mkuu mpya wa Benki, hatua inayolenga kuongeza uwezo wa kushughulikia miamala, kuimarisha usalama wa taarifa na kuwezesha utoaji wa huduma mpya kwa wateja zaidi ya milioni 10.

Mkurugenzi Mtendaji na Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB, Ruth Zaipuna, amesema mfumo huo umeandaliwa kwa zaidi ya miaka miwili kupitia majaribio, uhakiki wa teknolojia na tathmini za vihatarishi. Hatua ya mwisho ya kuhamisha taarifa za wateja ilianza Julai 31, 2026.

Mfumo huo unaunganisha akaunti, miamala, mikopo, matawi, mawakala, ATM, NMB Mkononi na huduma nyingine za benki. Zaipuna amewahakikishia wateja kuwa fedha, taarifa na kumbukumbu zao ziko salama, huku uendeshaji wa huduma ukiendelea kuimarika.

Uwekezaji huo unaweka msingi wa utekelezaji wa Mpango Mkakati wa NMB wa mwaka 2026–2030. Kwa sasa, benki hiyo ina matawi zaidi ya 250, mawakala zaidi ya 80,000, ATM zaidi ya 700 na zaidi ya misimbo 130,000 ya QR ya kupokea malipo.



Prev Post PITIA VICHWA VYA HABARI KATIKA MAGAZETI YA LEO AGOSTI 20, 2026 
Next Post Real Betis, Real Sociedad Mbinu na Takwimu Kuamua Leo
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook