Search
Sign In
2Your Cart
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

January Makamba Atoa Kauli ya Amani Baada ya Kutoteuliwa – Video

  • 48
Scroll Down To Discover

Mbunge wa Bumbuli anayemaliza muda wake na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC), January Makamba, amesema amekubaliana na uamuzi wa Kamati Kuu ya CCM wa kuondoa jina lake katika mchakato wa kuwania tena ubunge wa Jimbo la Bumbuli.

Makamba ametoa kauli hiyo siku chache baada ya Kamati Kuu ya CCM kutangaza majina ya wagombea ubunge kwa majimbo mbalimbali nchini, ambapo jina lake halikuwemo katika orodha hiyo ya awali.

“Kwenye CCM, dhana ya ‘kukatwa’ haipo. Ni aidha umependekezwa au umeteuliwa. ‘Kukatwa’ maana yake ni kwamba kuna nafasi unayostahili ambayo umeenguliwa, jambo ambalo si sahihi katika mfumo wetu,” alisema January Makamba.

“Wakati wa kuomba nafasi hizi, wote tunakuwa sawa – hakuna anayestahili zaidi ya mwingine. Kwa hiyo, hakuna dhana ya kukatwa. Ni aidha umependekezwa au hukupendekezwa; umeteuliwa au hukuteuliwa. Sisi hatukuteuliwa,” aliongeza Makamba.



Prev Post NAFASI 5 Za Security Officers Stamigold Company Limited
Next Post Zaidi ya asasi 167 kutoa elimu ya mpiga kura
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook