Search
Sign In
2Your Cart
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Muingereza: Elfyn Evans aibuka mshindi mbio za magari "Safari Rally" Kenya.

  • 57
Scroll Down To Discover

Dereva Elfyn Evans kutoka Uingereza ndiye mshindi wa mashindano ya mbio za magari ya Safar Rally ambazo zimekamilika mchana wa Jumapili hii, katika mji wa Naivasha nchini Kenya.

Evans mwenye umri wa miaka 36 ameshinda awamu hii ya tatu ya mashindano ya magari ulimwenguni WRC ambayo inatarajiwa kukamilika nchini Saudi Arabia mwezi Novemba, mwishoni mwa msimu wa 2025.

Evans na mwongoza njia wake waliongoza mashindano haya kuanzia siku ya pili hadi kukamilika kwa mashindano hayo kwenye mbuga ya Wanyama ya Hells Gate mjini Naivasha mwendo was saa tisa.

Rais wa Kenya William Ruto mbali na kuwapongeza madereva walioshiriki katika Makala ya mwaka huu ya Safari Rally, amesema kwamba; “ Kulingana na tunayoyasikia kwa walioshiriki ni kwamba mashindano ya mwaka huu yalikuwa makubwa zaidi na yaliwavutia madereva na mashabiki wengi katika eneo la mashindano,”

Mashindano ya Safari Rally Kenya , yalirejea kwenye msururu wa WRC miaka mitano iliyopita baada ya kuondolewa katika miaka ya tisini kwa ajili ya ukosefu wa maandalizi mema.

Huku Elfyn akifurahia ushindi wake wa kwanza kwenye Safari Rally, dereva mwenzake katika timu ya TOYOTA GAZOO WRT na mshindi mara mbili wa Safari Rally Kalle Rovapena, alilazimika kujiondoa kwenye mashindano katika kiwango cha 17- eneo la Olnegsengoni kwa ajili ya matatizo ya kiufundi kwenye gari lake.

Dereva wa Japani Takamoto Katsuta alipata ajali katika siku ya mwisho ambapo gari lake lilibingirika na japo aliweza kulirejesha barabarani na kukamilisha mashindano, hakuweza kujumuishwa katika orodha ya madereva kumi bora kwenye mashindano hayo.

Awali alikuwa na matumaini makubwa kuibuka mshindi .

Mashindano ya mwaka huu yalianza Alhamisi Machi 20th na Kukamilika Jumapili Machi 23 , muda yakiongezwa kwa siku moja ili kuwapa madereva muda wa kushiriki vyema.



Prev Post Bodi ya EWURA yakagua bomba la mafuta TAZAMA
Next Post Waislamu, Wakristo Burkina Faso Wala Futari Pamoja
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook