
MAGAZETI ya Leo Jumatano 04 May 2025
MAGAZETI ya Leo Jumatano 04 May 2025
Mbunge wa Viti Maalumu, Dk Tea Ntala ameitaka Serikali kupitia Wizara ya Afya kuchukua hatua za haraka kutoa elimu kwa umma kuhusu matumizi holela ya dawa ya dharura ya uzazi wa mpango (P2), akieleza kuwa tafiti mbalimbali zimebainisha madhara zaidi ya 10 yanayoweza kutokana na matumizi hayo.
Akichangia mjadala wa kupitisha makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Afya kwa mwaka wa fedha 2025/2026 bungeni jijini Dodoma leo Jumanne Juni 3, 2025 Dk Ntala amesema matumizi ya P2 yamekuwa yakiongezeka kwa kasi miongoni mwa vijana na wanawake bila uelewa wa kutosha kuhusu athari zake kiafya.
“Hizi P2, kwa sababu zinatumika hovyo, naomba mtoe elimu ya wazi kabisa, elimu ya wazi… nakuambia hiki kizazi kitapotea. Mabadiliko ya mzunguko wa damu, kiharusi… maana wanatumia hovyo, saratani ya kizazi na hata mimba kutoka… kuna madhara mengi kuliko faida,” amesema Dk Ntala.
Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!