Search
Sign In
2Your Cart
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Boni Yai: Mbowe Hana Uhusiano na Wanaojiondoa Chadema – Video

  • 29
Scroll Down To Discover

Kada maarufu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob almaarufu Boni Yai.

Kada maarufu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob almaarufu Boni Yai ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kanda ya Pwani ya chama hicho, amesema mwenyekiti mstaafu wa chama hicho, Freeman Mbowe hahusiki kwa namna yoyote na wanaojitoa kwenye chama hicho.

Mwenyekiti mstaafu wa chama hicho, Freeman Mbowe.

Boni Yai ameyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari Mei 18, 2025.

Hata hivyo ameeleza kuwa baadhi ya mambo yanayoendelea juu ya kukipinga chama hicho na misimamo yake pamoja na uongozi hayana baraka za Mbowe.

Kuithibitisha hilo Boniface ameeleza kuwa yeye binafsi Mbowe alimuarifu kuwa amezungumza na Katibu Mkuu wa CHADEMA John Mnyika na mazungumzo yao ilikuwa juu ya kama Mbowe anabariki mienendo ya baadhi ya watu wanaopinga msimamo wa chama.



Prev Post Waziri Mkuu Majaliwa Azindua Mradi wa Maji Hungumalwa Wilayani Kwimba
Next Post MAGAZETI ya Leo Jumatatu tarehe 19 May 2025
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook