Search
Sign In
2 Register
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Rais Mstaafu Dkt Jakaya Mrisho Kikwete Atunuku Tuzo Ya Chakula Barani Afrika

  • 5
Scroll Down To Discover

Rais Mstaafu wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Tuzo ya Chakula Barani Afrika kwenye hafla ya kutoa tuzop ya Chakula Barani Afrika kwa mwaka 2025 mjini Dakar, Senegal

Wanasayansi wanawake wawili – Profesa Mary Abukutsa-Onyango kutoka Kenya na Mercy Diebiru-Ojo kutoka Nigeria – wametangazwa washindi wa Tuzo ya Chakula Barani Afrika kwa mwaka 2025 (Africa Food Prize 2025).

Tuzo hiyo, yenye thamani ya Dola za Marekani 100,000, ilikabidhiwa na Rais Mstaafu wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Tuzo ya Chakula Barani Afrika.

Hafla ya kukabidhi tuzo ilifanyika mjini Dakar, Senegal, pembezoni mwa Jukwaa la Mifumo ya Chakula Afrika (AFSF) linaloendelea kuanzia tarehe 1 hadi 5 Septemba 2025.

Katika hotuba yake, Dkt. Kikwete aliwapongeza washindi kwa mchango wao wa kipekee katika tafiti zinazolenga kuongeza tija ya uzalishaji na kuboresha maisha ya wakulima wadogo barani Afrika.

Rais Mstaafu wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Tuzo ya Chakula Barani Afrika akiwatambulisha Profesa Mary Abukutsa-Onyango kutoka Kenya (kulia) na Mercy Diebiru-Ojo kutoka Nigeria ambao ni washindi wa Tuzo ya Chakula Barani Afrika kwa mwaka 2025 (Africa Food Prize 2025) kwenye hafla iliyofanyika mjini Dakar, Senegal, pembezoni mwa Jukwaa la Mifumo ya Chakula Afrika (AFSF) linaloendelea kuanzia tarehe 1 hadi 5 Septemba 2025.

“Tuzo hii inadhihirisha nafasi kubwa ya wanasayansi wa Afrika katika kutafuta suluhu za changamoto za kilimo. Ingawa mwaka huu imeenda kwa washindi wawili, tunatambua kazi kubwa inayoendelea kufanywa na watu binafsi na taasisi nyingi ili kuhakikisha bara letu linakuwa na mifumo imara na endelevu ya chakula,” alisema Dkt. Kikwete.

Profesa Abukutsa-Onyango amejikita katika tafiti za mboga mboga za asili za Kiafrika kama mchicha, sukuma wiki, mgagani, mchunga, figiri na kisamvu, akihamasisha uzalishaji na ulaji wake kwa madhumuni ya kuimarisha lishe.

Kwa upande wake, Mercy Diebiru-Ojo anasifika kwa kubuni na kuendeleza teknolojia ya kisasa ya uzalishaji na upandikizaji wa mbegu za mihogo kwa kutumia mbinu ya semi-autotrophic hydroponic technology, ambayo imeongeza mavuno na tija katika kilimo hicho muhimu barani Afrika.

Rais Mstaafu wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Tuzo ya Chakula Barani Afrika akiwa na Mwenyekiti wa AGRA NA Waziri Mkuu Mstaafu wa Ethiopia, Mhe Hailemariam Dessalegn na Profesa Mary Abukutsa-Onyango kutoka Kenya na Mercy Diebiru-Ojo kutoka Nigeria ambao ni washindi wa Tuzo ya Chakula Barani Afrika kwa mwaka 2025 (Africa Food Prize 2025) kwenye hafla iliyofanyika mjini Dakar, Senegal, pembezoni mwa Jukwaa la Mifumo ya Chakula Afrika (AFSF) linaloendelea kuanzia tarehe 1 hadi 5 Septemba 2025.

Tuzo ya Chakula Barani Afrika ilianzishwa mwaka 2005 chini ya mwamvuli wa mpango wa Mageuzi ya Kijani Afrika (AGRA). Inatolewa kila mwaka kwa watu binafsi au taasisi zinazotoa mchango wa kipekee katika kuimarisha mifumo ya chakula na maendeleo ya sekta ya kilimo.

Kwa mwaka huu 2025, jumla ya maombi 601 kutoka ndani na nje ya Afrika yaliwasilishwa kuwania heshima hii kubwa.



Prev Post CHAUMMA Jimbo la Segerea Kwazidi Kuwaka
Next Post Samia: Serikali ya CCM Inafanya Kazi kwa Kuheshimu Utu wa Mtanzania
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook