Search
Sign In
2Your Cart
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Watatu Wahofiwa Kufariki Ajali Ya Lori

  • 29
Scroll Down To Discover

Takribani watu watatu wanahofiwa kufariki dunia kufuatia ajali mbaya iliyotokea leo, Julai 7, 2025, katika eneo la Mtoni Msikitini, Temeke, jijini Dar es Salaam.
Ajali hiyo ilihusisha gari aina ya Toyota Land Cruiser lenye namba za usajili T617 DUL, ambalo lilipoteza mwelekeo na kugonga lori lenye namba T322 AVV, pamoja na Bajaj mbili na bodaboda mbili.


Inadaiwa kuwa watu waliopoteza maisha walikuwa wakisafiri kwa bodaboda zilizogongwa kwa nyuma na gari hilo, kisha kurushwa hadi kugonga lori.

Global TV imefika eneo la tukio na kushuhudia miili ikiondolewa barabarani, huku pia magari, Bajaj, na bodaboda zilizohusika kwenye ajali hiyo zikitolewa ili kuruhusu barabara, ambayo ilikuwa imefungwa kwa muda, ifunguliwe na magari yaendelee na safari.

Hadi sasa, mamlaka husika bado hazijatoa taarifa rasmi kuhusu idadi kamili ya waliopoteza maisha au hatua zilizochukuliwa kufuatia ajali hiyo.

Tufuatilie kupitia YouTube ya Global TV — usisahau ku-like, ku-comment na ku-subscribe ili uendelee kuhabarika kila siku kwa habari mbalimbali zenye ukweli na uhakika.



Prev Post Milio ya bunduki, mabomu yasikika Nairobi
Next Post NECTA Yatangaza Matokeo Ya Kidato Cha Sita
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook