Search
Sign In
2 Register
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

NMB YAPANUA MALIPO YA KIDIJITALI KARIAKOO FESTIVAL

  • 8
Scroll Down To Discover

Wafanyabiashara wa Kariakoo wanatarajiwa kupata fursa zaidi za mauzo na kupokea malipo kwa njia za kidijitali kupitia Kariakoo Festival 2026. Benki ya NMB imetangaza udhamini wa Sh milioni 165 kwa tamasha hilo litakalofanyika Septemba 25 hadi 27 katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam.

Msimu wa tatu wa tamasha hilo ulizinduliwa Septemba 8 kwa msafara maalumu uliopita katika barabara na mitaa mbalimbali ya Kariakoo kabla ya kuishia Soko Kuu la Kariakoo. Uzinduzi uliongozwa na Meneja Mkuu wa Shirika la Masoko ya Kariakoo, Ashraph Abdulkarim, kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Edward Mpogolo.

Mkuu wa Idara ya Biashara wa NMB, Alex Mgeni, alisema wafanyabiashara watapata huduma za kupokea malipo kupitia NMB Lipa Namba na NMB Mkononi. Watapata pia nafasi ya kutumia NMB Tap pamoja na taarifa kuhusu Mshiko Fasta na NMB SME World Business Credit Card kwa ajili ya mahitaji ya mitaji.

Abdulkarim alisema tamasha hilo litawasaidia wafanyabiashara kuuza bidhaa kwa bei za punguzo na kupunguza mizigo iliyopo maghalani kuelekea mwisho wa mwaka. Waandaaji wamewahimiza wafanyabiashara kujisajili mapema na wanunuzi kujitokeza kwa wingi.



Prev Post PITIA VICHWA VYA HABARI KATIKA MAGAZETI YA LEO SEPTEMBA 09, 2026 
Next Post Fei Toto Agoma Kuzungumzia Yanga na Simba, Aweka Wazi Mkataba Wake Azam FC
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook