Search
Sign In
2 Register
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Serikali Yavunja Ukimya Ripoti ya CNN: “Tunachambua Maudhui Kwa Umakini”

  • 27
Scroll Down To Discover

Mwandishi wa CNN, Larry Madowo

SERIKALI ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imesema imefuatilia makala iliyochapishwa muda mfupi uliopita na chombo cha habari cha CNN kuhusu matukio ya tarehe 29 Oktoba, 2025 na siku zilizofuata.

Taarifa ya leo Novemba 21, 2025 iliyotolewa na Katibu Mkuu, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa imesema “Tunachambua na kuhakiki maudhui yaliyomo katika makala hiyo na tamko la Serikali litakuja baada ya kukamilika kwa uhakiki huo.”

Katibu Mkuu, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa imesema.

Mapema leo Novemba 21, 2025, CNN ilitoa ripoti ya uchunguzi wake wa kina ambapo imedai imebaini ushahidi unaoonyesha kuwa Polisi wa Tanzania walitumia risasi kuwashambulia na kuwaua waandamanaji waliokuwa wakipinga Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29.

Ripoti hiyo ya CNN ikiongozwa na mwandishi Larry Madowo imedai imeufanya uchunguzi huo kwa uchambuzi wa forensic, ikiwemo muunganiko wa video, picha za maeneo ya tukio, na picha za satelaiti.



Prev Post Benki Ya Stanbic Yatoa Vifaa Tiba Kituo Cha Afya Goba
Next Post Matatizo ya Afya Yanayosababishwa na Maji Kupita Kiasi Mwilini
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook