Search
Sign In
2 Register
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Kesi ya Luhaga Mpina Yatupiliwa Mbali, NEC Yapewa Uhalali wa Maamuzi Yake

  • 2
Scroll Down To Discover

Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu Dodoma, leo Jumatano Oktoba 15, 2025, imetupilia mbali kesi iliyofunguliwa na Luhaga Mpina na chama cha ACT-Wazalendo kupinga uamuzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) wa kumuengua Mpina katika nafasi ya kugombea urais kwenye Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2025.

Jopo la majaji watatu likiongozwa na Jaji Fredrick Manyanda, likisaidiwa na Majaji Sylvester Kainda na Abdallah Gonzi, limeeleza kuwa kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Sheria za Uchaguzi, NEC ni chombo huru kisichopaswa kuingiliwa na mahakama au taasisi nyingine endapo limefanya maamuzi yake kwa nia njema na kwa kufuata taratibu.

Mahakama imeeleza zaidi kuwa hoja zilizowasilishwa na upande wa walalamikaji hazikuonyesha ukiukwaji wa haki za msingi wala ushahidi wa upendeleo katika mchakato wa kuenguliwa kwa Mpina.

Kwa uamuzi huo, Luhaga Mpina hataweza kushiriki katika kinyang’anyiro cha urais mwaka huu, huku kampeni za vyama vingine vinavyoshiriki uchaguzi huo zikiendelea kote nchini.

MWANDISHI AMBANANISHA MULIRO KUHUSU ALIPO POLEPOLE – AJIBIWA kwa HOJA – ”SITARAJII KUBISHANA”….



Prev Post Kesi ya Uhaini ya Tundu Lissu Yahirishwa Kufuatia Msiba wa Naibu Msajili wa Mahakama Kuu
Next Post Uwanja wa Sokoine Wafungwa Kutumika Kwa Mechi za Ligi
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook