Search
Sign In
2 Register
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

UN Yasisitiza: Vita Ghaza Lazima Vikome, Hamas Waachilie Mateka

  • 4
Scroll Down To Discover

Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UN), Annalena Baerbock ameuambia mkutano wa suluhisho la mataifa mawili uliofanyika makao makuu ya umoja huo jana Jumatatu: kuwa “nchi-dola huru ya Palestina lazima ianzishwe”.

Baerbock akaongeza: “hali halisi ya watoto wa Ghaza ni vita na uharibifu. Wengi wameuawa huko Ghaza bila ulimwengu kujua majina yao.”

Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa amefafanua katika hotuba yake hiyo kwa kusema: “ulimwengu umewaangusha watoto wa Ghaza. Watoto wote katika Mashariki ya Kati wanastahili kuishi”.

Katika sehemu nyingine ya hotuba yake, Baebock amesema: “tunahitaji usitishaji vita wa haraka na bila masharti huko Ghaza. Hamas lazima iwaachilie mateka wote mara moja na bila masharti”.

Rais huyo ni Waziri wa zamani wa mambo ya nje wa Ujerumani amewaeleza washiriki wa mkutano wa suluhisho la nchi-dola mbili: “hali ya kutisha ya Gaza inaonyesha kwamba hatuwezi kuruhusu uharibifu kama huo utokee tena. Hali ya Ghaza haikubaliki na vita lazima vikome”.

Baerbock amesisitiza kwa kusema: “nchi huru na endelevu ya Palestina lazima ianzishwe. Hamas inapaswa kuweka chini silaha zake na kuhitimisha utawala wake huko Ghaza”. Rais wa sasa wa Palestine ni Mahmoud Abbas

MADEREVA 15 WAKAMATWA, LESENI 7 ZAFUTWA KATIKA OPERESHENI KALI YA TRAFIKI….



Prev Post Mgombea Mwenza wa CCM Aendeleza Kampeni kwa Kishindo Njombe Mjini
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook