Search
Sign In
2 Register
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

MAMBO YA FOLZ HUKO YANGA MHHHH…..ALI KAMWE ‘ACHANA JAMVI’ MAPEMA….

HATMA ya Kocha Mkuu wa Yanga, Romain Folz, kuendelea na kibarua cha kuinoa timu hiyo au la itajulikana leo baada ya uongozi wa klabu hiyo kutoa matokeo ya tathimini iliyofanywa kuhusu benchi la ufundi. Ofisa Habari wa Klabu hiyo, Ali Kamwe, jana alisema uongozi chini ya Kamati ya Utendaji, umemaliza kufanya tathmini hivyo wakati wowote kuanzia leo wanatarajia kutangaza matokeo yake pamoja na kufanya maboresho kidogo. Uongozi wa Yanga ulifanya tathmini hiyo kutokana na mlalamiko ya baadhi ya wanachama na mashabiki kuhusu kiwango cha timu yao, ingawa timu imekuwa ikipata matokeo mazuri. Baadhi wanadai timu haichezi soka la kuvutia kama ilivyokuwa misimu mitatu iliyopita, hivyo kutokuwa na imani na kocha Folz, ambaye ameichukua timu hiyo kutoka kwa Miloud Hamdi, aliyetimkia, Ismailia ya Misri. “Hapa kati kumekuwa na maneno mengi kuhusu kiwango cha timu, mara ya mwisho hivi karibuni nilieleza kwa wanachama na mashabiki kwamba kuna tathmini ambayo uongozi wa klabu inaufanya, niliwaahidi baada ya kufanyika nitarudi kuwaleza ni nini viongozi wamekiamua. “Niko hapa kuwaambia wanachana na mashabiki kuwa tathmini imekamilika, yako maboresho kidogo ambayo yamefanywa kwenye benchi la ufundi kwa hiyo wakati wowote kuanzia sasa tunaweza kuwatangazia, tunaweka utaratibu sawa tu, lakini kila kitu kimeshakamilika,” alisema. Aliwataka wanachana na mashabiki kuwa tayari kupokea taarifa ya tathmini pamoja na maboresho hayo kwa manuafaa ya timu yao pamoja na kuyaunga mkono. “Kwa maana hiyo wanachama na mashabiki wa Yanga wawe tayari na taarifa tutakayoitoa, waone ni kitu gani ambacho uongozi wao umekifanya na maboresho gani yamefanyika,” alisema. Siku chache zilizopita, Kamwe, alibainisha kuwapo kwa tathimini iliyoanzishwa na viongozi, lakini akadai inafanywa kwenye idara zote ikiwamo yao pia. “Tathimini inafanyika, lakini siifanyi mimi, inafanywa na Kamati ya Utendaji kwa kushirikiana na idara mbalimbali na hiyo si ya kocha tu au benchi la ufundi, ni ya taasisi nzima inayokwenda kwenye idara mbalimbali, ikiwamo hii ya habari na mashindano ya wanachama,” alisema Kamwe wakati kamati hiyo ilipokuwa inaendelea na tathimini hiyo. Wakati hayo yakiendelea kikosi cha timu hiyo jana kimeingia kambini rasmi kujiandaa na mchezo wa mkondo wa kwanza, Ligi ya Mabingwa Afrika, raundi ya kwanza dhidi ya Silver Strikers ya Malawi. Habari zinasema kabla ya hapo wachezaji walikuwa wanafanya mazoezi na kurudi nyumbani, ikiwamo mchezo wa kirafiki dhidi ya TRA United, uliochezea katikati ya wiki iliyopita, Uwanja wa Gymkhana, Dar es salaam na kutoka suluhu. Mechi hiyo inatarajiwa kupigwa, Jumamosi ijayo, saa 10:00 jioni, Uwanja wa Bingu Mutharika, Lilongwe nchini Malawi. Kikosi cha timu hiyo kinatarajiwa kuondoka wakati wowote kuanzia kesho, huku zaidi ya mabasi 20 ya mashabiki yakitarajiwa kuondoka kwa njia ya barabara kuifuata timu hiyo kwa ajili ya kuipa sapoti. “Niwapongeze wanachana na mashabiki wa Yanga wa Mbeya na Iringa, wameonekana kuhamasika zaidi kwenda nchini Malawi. “Dar es Salaam nao naona mwamko umeanza kuwa mkubwa, watu waendelee kujitokeza kwa ajili ya safari,” alisema Kamwe. The post MAMBO YA FOLZ HUKO YANGA MHHHH…..ALI KAMWE ‘ACHANA JAMVI’ MAPEMA…. appeared first on Soka La Bongo.

Kenya yaomboleza kifo cha Raila Odinga. Dira ya Dunia TV

Aliyekuwa waziri mkuu wa Kenya na kinara wa chama cha ODM Raila Odinga ameaga dunia. Kwa mujibu wa taarifa iliyowasilishwa na Rais William Ruto mapema leo, Raila alifariki alipokuwa akipokea matibabu katika hospitali ya Devamatha iliypo mjini Keralla nchini India. #RailaOdinga #Kenya #bbcswahili Subscribe kupata video motomoto kila siku kutoka BBC Idhaa ya Kiswahili https://www.youtube.com/channel/UCoerKKIKIMlDYaVFSTlsWGw

NMB YAFADHILI ZIARA YA KIBIASHARA YA WAJASIRIAMALI 28 NCHINI CHINA

Na Mwandishi Wetu Benki ya NMB imefadhili ziara ya kibiashara ya wafanyabiashara 28, ambayo inalenga kuwapa uzoefu wa moja kwa moja wa masoko ya China na kuwaonesha fursa za biashara za kimataifa. Ziara hii ni sehemu ya jitihada za benki hiyo kuimarisha ushindani wa wateja wake katika soko la kimataifa na kuwasaidia kupata maarifa muhimu kuhusu mnyororo wa usambazaji, mbinu za upatikanaji wa bidhaa, na kukuza ushirikiano na wawekezaji wa China. Ili kuhakikisha ufanisi stahiki unapatikana, wajumbe wa msafara huo watatembelea maeneo mbalimbali vikiwemo viwanda, vituo vya biashara, pamoja na taasisi za Serikali na sekta binafsi, kwa lengo la kujifunza, kubadilishana uzoefu, na kuibua fursa za ushirikiano na maendeleo. Akizungumza katika hafla ya kuwaaga wafanyabiashara hao iliyofanyika Jumatatu jijini Dar es Salaam, Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara wa Benki ya NMB, Bw. Filbert Mponzi, alieleza kuwa ziara hiyo ya siku tisa, inayotarajiwa kuanza leo, itajumuisha pia kushiriki katika Maonyesho ya 138 ya Biashara ya Kimataifa ya Canton, ambayo ni miongoni mwa maonesho makubwa na yenye mvuto mkubwa duniani. “Ziara hii ni fursa adhimu kwa wafanyabiashara wetu kujipatia maarifa mapya, kufungua milango ya masoko ya kimataifa, na kujifunza mbinu bora na za kisasa za uendeshaji wa biashara. Ujuzi huu utasaidia si tu kukuza biashara zao binafsi, bali pia kuchangia kikamilifu katika maendeleo ya uchumi wa taifa,” alibainisha Bw Mponzi. Aidha, aliongeza kwa kusema: “Hii ni mara ya tano tangu mwaka 2019 kwa Benki ya NMB kuandaa na kufanikisha ziara ya kimataifa ya mafunzo kwa wateja wake. Msafara wa mwaka huu ni mkubwa zaidi kuwahi kufadhiliwa na benki yetu, jambo linalotufanya kuwa na matarajio makubwa katika kuleta matokeo chanya yatakayodhihirisha thamani ya uwekezaji huu.” Bw Mponzi alifafanua kuwa kundi la mwaka huu lina wawakilishi 12 kutoka mnyororo wa thamani wa kilimo kutokana na umuhimu wa sekta hiyo katika uchumi wa taifa, huku 16 wengine wakitoka sekta mbalimbali. Baadhi ya wafanyabiashara walioteuliwa kushiriki katika ziara ya mwaka huu wameeleza kuwa safari hiyo si tu inawapa fursa ya kupata bidhaa zenye ubora wa kimataifa, bali pia maarifa muhimu ya kuongeza ubunifu, kuboresha mifumo ya uendeshaji wa biashara, na kuelewa kwa undani mahitaji na mwelekeo wa soko la dunia.. “NMB imetufungulia milango ya ndoto zetu. Kupata nafasi kama hii ya kukutana ana kwa ana na wazalishaji wakubwa wa China ni fursa adimu,” alisema Bw Sanjay Sumariya wa Singida Kilimo Ltd. Bi Delfina Leon kutoka Barefoot International alisema kuwa anatarajia kujifunza zaidi kuhusu viwango vya ubora wa bidhaa, utaratibu wa kuagiza kwa wingi, na fursa za ushirikiano wa muda mrefu na kampuni za China. Kwa upande wake, Bw Award Assah Mpandilah, aliyeshiriki kwenye ziara ya kwanza mwaka 2019, alieleza namna ilivyobadilisha mwelekeo wa biashara na maisha yake. “Nilirejea nikiwa na mtazamo mpya kabisa wa kibiashara. Kupitia ziara hiyo, niliweza kuanzisha mahusiano ya moja kwa moja na wawekezaji, ambao hadi leo tunaendeleza ushirikiano wenye mafanikio makubwa yote haya yakiwa ni matokeo ya maono na uwekezaji wa NMB katika kuwawezesha wateja wake,” alieleza. Utaratibu huu wa NMB unaendana na ajenda ya Serikali ya kuimarisha sekta binafsi, kupanua wigo wa bidhaa na huduma za Tanzania katika masoko ya kimataifa, pamoja na kuvutia uwekezaji wa kigeni kupitia ushirikiano wa kimkakati na wenye tija. “Kwa kutoa fursa kama hizi” alisema Bw David Mdeka wa Mafinga, “Benki ya NMB inaendelea kuonesha dhamira yake kwa kuwa taasisi ya fedha na mshirika wa kweli wa maendeleo ya wateja wake na taifa kwa ujumla.”

SHUJAA ANAPOTEZA KILA KITU KWA KUANGUKIA PENZINI NA KIJAKAZI

🎬 Movie Title: THE RISE OF IGBINOGUN 🎞️ Genre: Drama 📺 Watch Full Movie On NETFLIX Produced By Onesoul _____________________________________ At E7Bits, we do short recaps to help Swahili-speaking audiences enjoy and understand African movies better. We DON’T own the movies — we promote them with respect. 📩 For takedown or promo requests, contact us via: e7bitscrew@gmail.com Hit Us Up: +255624944364 ______________________________________ Background Music Credits Alex Productions - ‘Elite’ is under a Creative Commons (BY 3.0) license: https://creativecommons.org/licenses/by/3.0/ / @alexproductionsnocopyright Music powered by BreakingCopyright: https://youtu.be/0Q7QpKVUlc8?si=GqQ9Znoueq-LVZxG #zeelakutune #zeelatown #e7bits #izkonka

The Roughneck (2025)

An oil worker and his dog embark on a journey to his wedding, but after a violent attack at a rest stop, he teams with his ex-convict father to seek revenge, uncovering dark secrets in their rural community. The Roughneck (2025) Genre: Thriller, Action, Drama Release Date: 2025 Stars: Austin North, Holt McCallany, Dichen Lachman, La Monde Byrd, Brook Sill Language: English Runtime: 91 mins

AGNESS SULEIMAN KAHAMBA (AGGYBABY ) ASHINDA TUZO YA MWIGIZAJI BORA WA KIKE WA TANZANIA MWAKA 2025 

Msanii wa Muziki na Maigizo Bi Agness Suleiman Kahamba maarufu kama (Aggybaby) amepokea Tuzo ya Mwigizaji Bora wa Kike wa Mwaka 2025 kutoka Achievers Awards International ya nchini Nigeria kutokana na kazi zake za sanaa ya uigizaji na shughuli zake za huduma kwa jamii kupitia taasisi yake—Tupaze Sauti Foundation (Tanzania).  Waandaaji wa tuzo hizi wametambua kazi nzuri anayoifanya mwanatasnia Agness katika sekta ya filamu hususani kupitia tamthiliya za “Panguso”, “Huba” na kazi zake nyingine za filamu katika mtandao wa YouTube.  Tuzo hii ni alama ya ushirikiano wa kifilamu uliodumu kwa muda mrefu kati ya Tanzania na Nigeria .Bi Agness amebainisha kwamba waandaaji wa tuzo hizi wanavutiwa sana na filamu kutoka Tanzania kipekee wautaja utamaduni wetu, amani na ushirikiano unaooneshwa katika filamu zetu kuwa alama ya utu wa mwafrika—akinasibisha yale wanayoyaona kupitia tamthiliya ya “Kombolela”. Leo, Jumatatu Tarehe 13 Oktoba 2025—Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania, Dkt. Gervas Kasiga (PhD) amekutana na kufanya mazungumzo na mwatasania wa filamu na michezo ya kuigiza nchini—Agness Suleiman Kahamba @aggybaby__ Pia Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Dkt. Gervas Kasiga (PhD) amempongeza Agness kwa juhudi zake za kufanya kazi bora za filamu na kwa kuiwakilisha vyema Tanzania katika majukwaa ya filamu kimataifa.  Aidha, Dkt. Kasiga (PhD) amemsihi Agness kuendelea kufanya kazi zake za sanaa kwa ubunifu na weledi mkubwa ili kuutangaza vyema utamaduni wetu wa Kitanzania ndani na nje ya mipaka ya nchi yetu.


Deprecated: strip_tags(): Passing null to parameter #1 ($string) of type string is deprecated in /home/bongonet/domains/bongonet.co.tz/public_html/index.php on line 109

MANNAT 1-140|VASCO DJ

#mbosso #pawa # #photoshoot

Enjoy the videos and music you love, upload original content, and share it all with friends, family, and the world on YouTube.

PITIA VICHWA VYA HABARI KATIKA MAGAZETI YA LEO OKTOBA 16, 2925

Ajebutter22 – Gbe Kini Yen Ft. Minz & Boj

MAMBO YA FOLZ HUKO YANGA MHHHH…..ALI KAMWE ‘ACHANA JAMVI’ MAPEMA….

Kenya yaomboleza kifo cha Raila Odinga. Dira ya Dunia TV

NMB YAFADHILI ZIARA YA KIBIASHARA YA WAJASIRIAMALI 28 NCHINI CHINA

Nissah – Ex Pole

SHUJAA ANAPOTEZA KILA KITU KWA KUANGUKIA PENZINI NA KIJAKAZI

The Roughneck (2025)

AGNESS SULEIMAN KAHAMBA (AGGYBABY ) ASHINDA TUZO YA MWIGIZAJI BORA WA KIKE WA TANZANIA MWAKA 2025 

Marioo & Element Eleéeh – Njozi

MANNAT 1-140|VASCO DJ

#mbosso #pawa # #photoshoot

Udi – Shobo sitaki

Loading views...
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook