Search
Sign In
2Your Cart
Your Cart 2 items
Subtotal : $1559

Trump Afanyiwa Uchunguzi wa Kiafya, Adhibitika Kuwa na Tatizo la Mishipa ya Damu

  • 37
Scroll Down To Discover

Rais wa Marekani Donald Trump (79) amefanyiwa uchunguzi wa kiafya baada ya kubainika kuwa na uvimbe mdogo kwenye miguu yake, hali ambayo madaktari wake wameithibitisha kuwa ni matokeo ya chronic venous insufficiency, yaani kushindwa kwa mishipa ya damu kurudisha damu vizuri kuelekea kwenye moyo.

Taarifa hiyo imesomwa na msemaji wa Ikulu ya White House, Karoline Leavitt, kupitia barua rasmi iliyotolewa na daktari wa rais, Kapteni Sean Barbabella.

Kwa mujibu wa daktari Barbabella, Trump alifanyiwa vipimo vya kina, ikiwa ni pamoja na uchunguzi wa Doppler wa mishipa ya miguu, ambao ulithibitisha kuwepo kwa hali hiyo isiyo ya hatari. Daktari huyo aliongeza kuwa ni jambo la kawaida kwa watu wenye umri wa zaidi ya miaka 70.

“Hakuna dalili yoyote ya ugonjwa wa kuganda kwa damu kwenye mishipa mikubwa, wala maradhi ya moyo, figo, au ugonjwa mwingine wa mwilini,” amesema Kapteni Barbabella.

Daktari huyo amesema hali ya Trump inadhibitiwa vyema na haina athari kwa majukumu yake ya kila siku kama Rais wa Marekani.https://youtu.be/mhHAfPndYNE



Prev Post Ruto: Wapinzani hawana mipango ya ajira, wanachochea vurugu
Next Post Polisi Wachunguza Tukio la Utekaji na Urejeo wa Mwanamke Bahari Beach
Related Posts
Comments 0

    Hakuna maoni bado. Kuwa wa kwanza kuandika maoni!

Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook