Jinsi kijiji kidogo kilivyogeuka kuwa mji mkuu wa YouTube

  • 63
Scroll Down To Discover

Tulsi, kijiji kilicho katikati mwa India, kimeibua mapinduzi ya kiuchumi na kijamii kupitia mitandao ya kijamii, hasa mtandao wa YouTube.
Tulsi ni kijiji chenye nyumba za ghorofa moja na barabara pana za vumbi. Tangi la kuhifadhia maji likitazama mji. Pesa ambazo watu huzipata kupitia YouTube zimebadilisha uchumi wa kijiji, wenyeji wanasema.
Wakazi ambao wameunda chaneli za YouTube na kujipatia mapato ni pamoja na wanawake ambao hapo awali walikuwa na fursa chache za kujiendeleza katika mazingira haya ya mashambani.
Takribani watu 4,000 wanaishi Tulsi, na ripoti zinaonyesha zaidi ya 1,000 hutengeneza maudhui kwa ajili ya YouTube. Ukitembea katika kijiji chenyewe, ni ngumu kupata mtu ambaye hajaonekana katika mojawapo ya video zinazorekodiwa.
Februari 2025 ni kumbukumbu ya miaka 20 ya YouTube. Takribani watu bilioni 2.5 hutumia jukwaa hili, na India ni mojawapo ya soko kubwa la YouTube kufikia sasa.
"Inawaweka watoto mbali na tabia mbaya na uhalifu," anasema Netram Yadav, 49, mkulima huko Tulsi na mmoja wa watu wanaovutiwa na ushiriki wa kijiji hicho katika mitandao ya kijamii.



Prev Post UN: Vita DRC ‘Imezalisha’ Wakimbizi 100,000
Next Post Diamond kutambulisha msanii mpya Wcb Wasafi
Related Posts
Comments 1
Leave A Comment
or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook